The House of Favourite Newspapers

ROSTAND SHUJAA, APANGUA PENALTI TATU, AIPELEKA YANGA 16 BORA


KIPA Youthe Rostand ameibuka shujaa baada ya kupangua penalti 3 na kuiwezesha Yanga kuibuka na ushindi wa mabao 4-3 dhidi ya Ihefu ya Mbeya.
Yanga ilikuwa ikiivaa Ihefu katika mechi ya Kombe la Shirikisho iliyochezwa kwenye Uwanja wa Sokoine mjini Mbeya, leo. Kipa huyo wa Cameroon amepangua mikwaju mitatu ya penalti wakati wa changamoto za mikwaju hiyo. Yanga wameibuka na ushindi wa jumla ya 6-5.
Al manusura Yanga ing’olewe baada ya Obrey Chirwa kukosa penalti, lakini kipa huyo Mcameroon akapangua penalti iliyofuata na kuifanya Yanga iendelee.
Yanga ililazimika kuingia kwenye changamoto hizo na timu hiyo ya daraja la pili baada ya kusawazisha katika dakika za majeruhi baada ya kuwa imefungwa bao. Chirwa ndiye aliyesawazisha kwa mkwaju wa penalti huku Ihefu wakiwa wanaamini mechi ilikuwa imeisha.

Global Publishers App imekurahisishia kutazama matokeo ya kidato cha nne kupitia simu ya mkononi. Install Global Publishers sasa uyasome yote: Bofya  au 

Comments are closed.