Mkurugenzi wa Samsung Afrika, Hong Seok akizungumza na wanahabari (hawapo pichani) kushoto ni Mkurugenzi wa duka hilo, Happy Grayson.Watumiaji wa bidhaa za Samsung, leo wameendelea kusogezewa huduma baada ya Kampuni hiyo kufungua duka jipya la bidhaa zake mbalimbali, katika makutano ya Sanamu ya Sskari Posta jijini Dar es Salaam ambalolimepewa jina la Samsung Askari Samora.
Duka hilo lenye bidhaa mbalimbali za kampuni hiyo ikiwemo simu, majokovu, majiko, vipoza hewa ‘air condition’ televisheni, pasi na nyinginezo.
Katika uzinduzi huo Mkurugenzi wa duka hilo, Happy Grayson amesema duka hilo litauza bidhaa za Samsung Orijino na kila mnunuzi atapata punguzo la asilimia tano.
PICHA: RICHARD BUKOS / GPL
Comments are closed.