The House of Favourite Newspapers

Seneta Mbaroni kwa Mauaji ya Rais

0

MAMLAKA nchini Jamaica imemkamata Seneta wa zamani wa Haiti Bw. John Joel Joseph kama mshukiwa namba moja wa mauaji ya Rais wa zamani wa Haiti Jovenel Moise.

 

Rais Moise aliuawa tarehe 7 Julai Mwaka jana na watu wenye silaha waliovamia nyumbani kwake katika mji mkuu wa Haiti, Port-au-Prince.

 

Mara baada ya mauaji hayo, Kiongozi mmoja wa juu wa Polisi nchini humo alitoa taarifa kuwa Bw. Joseph ndiye aliyewapatia silaha majambazi hao na pia alifanya nao mikutano kadhaa. Bw. Joseph alikamatwa juzi.

Leave A Reply