MKURUGENZI Mtendaji wa Kampuni ya Global Group, Eric Shigongo amehudhuria hafla ya sherehe ya mpwa wake aitwaye, Emmanuel Aron.
Hafla ya sherehe hiyo inafanyika usiku huu baada ya mchana kufungwa kanisa la Katoliki la Nundu- Meco na inafanyika ndani ya ukumbi wa Hoteli ya Gold Crest ya Jijini Mwanza.
Shigongo akimuasa mpwa wake amesema kuwa familia yao ipo imara katika kuhakikisha familia ya Emmanuely na Christina inakuwa katika misingi ya dini na ya kumpendeza mwenyezi mungu.
Alisema kuwa hategemei kuona mpwa wake Emmanuel akimbadilikia mkewe na ahakikishe wanavumiliana kwa shida na tabu kama maandiko yasemavyo, yeye hatasita kuwasaidia pale patakapohitajika msaada.
Comments are closed.