STORI: ANDREW CARLOS, IJUMAA WIKIENDA
DAR ES SALAAM: Ama kweli Januari ni mwezi dume! Staa wa sinema za Kibongo, Skyner Ally ‘Skaina’ juzikati amenaswa laivu ndani ya Klabu ya Maisha Basement, Kijitonyama jijini Dar akinywa kilevi kikali ‘ngumu kumeza’ bila wasiwasi tofauti na alivyozoeleka kupiga vitu laini.
Likiwa ndani ya kiota hicho cha burudani usiku wa manane, Wikienda lilimshuhudia Skaina akizama ukumbini hapo akiwa ameongozana na mashosti zake kwa ajili ya kula bata ndefu kama kawaida yao.
Wakati shoo ikiendelea, Skaina yeye alikuwa hana habari na mtu zaidi ya kuendelea kushikilia glasi iliyokuwa na ngumu au konya huku akiinywa kana kwamba anaombea mwezi huu dume uishe tu kwa amani aanze kunywa vitu laini.
Kuna muda alivamiwa na wenzake mahali alipokaa kisha wakaanza kutandika ngumu kila mmoja huku kila mmoja akiupigia saluti Mwezi Januari kwani mastaa wengi huwa wakienda maeneo ya starehe hupendelea kunywa vitu laini lakini sasa hivi ngumu kumeza ndiyo mpango mzima kwani inanyweka kidogo na kulewesha zaidi.
Wikienda lilimtimbia Skaina na kumuuliza kulikoni kunywa ngumu kumeza ambapo aliomba kuachwa kwani yupo kwenye starehe zake binafsi.
Comments are closed.