SPOTI XTRA ALHAMISI LAANZA KWA KISHINDO – PICHAZ
HAYAWIHAYAWI hatimaye yamekuwa, baada ya maombi ya muda mrefu ya wasomaji wetu, Gazeti Bora la Michezo nchini, Gazeti la Spoti Xtra leo Alhamisi, Septemba 20, 2018 limeanza kutoka mtaani mara mbili kwa wiki, yaani kila Alhamisi na Jumapili.
Wafanyakazi wa Global Publishers wakiongozwa na Mhariri Mtendaji, Saleh Ally, wametinga mtaani katika maeneo ya Ubungo, Mawasiliano, Makumbusho na sehemu nyingine za Jiji la Dar es Salaam kuuza Gazeti la Spoti Xtra sambamba na kuwaelimisha ubora wa gazeti hilo na vitu vilivyomo ndani yake.
Spoti Xtra limesheheni takwimu za soka na michezo mbalimbali inayopendwa duniani, uchambuzi makini wa mechi na masuala ya michezo bila kusahau ratiba na matokeo ya ligi zote kubwa duniani.
Aidha, Spoti Xtra limesheheni makala za kuvutia za michezo, stori za burudani na mastaa wa ndani na nje ya nchi.
Unaambiwa kwamba, Spoti Xtra linakupa uhondo zaidi kwa #Jero, pia linakupa fursa ya kushinda zawadi kibao zikiwemo jezi orijino za timu za Ulaya uzipendazo.
Wapenzi wa michezo wamestuka, hawaendi kwingine, bali ni Spoti Xtra pekee, mwambie na mwenzako, #SpotiXtra ndo’ habari ya mjini.
Ndani yake kuna kuponi itakayokupa nafasi ya kushinda zawadi kibao, hujachelewa #SpotiXtra #HapaNiUhondoTu kila Alhamisi na Jumapili.
PICHA NA SWEETBERT LUKONGE | GLOBAL PUBLISHERS
Comments are closed.