The House of Favourite Newspapers

T.I ATEULIWA KUSAIDIA JAMII HAKI ZA WAFUNGWA NA MAGEREZA

Image result for T.I

RAPA kutoka pande za  Mrekani Clifford Joseph Harris Jr almaarufu T.I, imelipotiwa kuwa miongoni mwa watu walioteuliwa kuisaidia jamii hasa kwenye masuala ya haki za wafungwa na magereza ya Atlanta nchini Marekani.

Kwa mujibu wa mtandao wa US News, Inaelezwa kuwa mji huo umeteua jumla ya watu 25 akiwepo na T.I huku jukumu kubwa la watu walioteuliwa ni kuzisaidia jela za mji huo ambazo uhifadhi watu wanaovunja sheria ndogo ndogo na kanuni za Atlanta.

Inatajwa kuwa kikao cha kwanza kwa ajili ya kushauriana vitu vya kufanya kitafanyika Julai 16, 2019 na mapendekezo watakayo kuwa nayo yatafikishwa kwa Meya wa mji huo Bi Keisha Lance  ambapo yatapitiwa na kupitishwa.

Comments are closed.