The House of Social Media
gunners X
Browsing Tag

makala maisha

Kataa kuwa mpira wa kona

JUMATANO saafi , Shangingi wenu nimejaa tele kuwaletea ile kitu roho inapenda. Niwape maneno yenu pambe, niwachambe vizabizabina msio na haya wala hamjui vibaya. Kuna tabia za baadhi ya wanawake huwa najiuliza wamezaliwa au wametupwa…

Utamu wa pipi mate yako!

WAPE habari wenye habari zao. Shangingi Mstaafu nakuja kifua mbele kuwapa maneno pambe, si mnanijua vizuri eeeh! Mwaka ndio huo unaanza, wanawake mjitambue sasa!  Mwanamke ujitunze uolewe sio kudanga tu miaka nenda rudi…

Moto hafunikwi shuka

MIMI sihitaji mkeka; kwani nataka kuswali? Miye hata chini naketi, kikubwa ujumbe ukufike bibiye upooo!?  Kuna mwenzenu mmoja kaninukisha shombo, basi hapa najisikia kichefuchefu cha hatari; na kama mjuavyo pa kutapikia sina…

MNAOCHAGUA WA KUWAOA SOMENI HII

ZAMA hizi ni za kusaidiana kwa kila kitu. Kama wewe ni binti ambaye unatamani na unataka ukute au upate mwanaume wa kukuoa akiwa na kila kitu bila wewe kuvuja jasho au kushiriki, utasubiri sana. Utaendelea kulalamika kuwa hakuna waoaji…

Dela la kuazima Halichafuki

WANAKWAMBIA ndege wafananao huruka pamoja nashanga wee bundi sijui utaruka na nani? Hehe heeeiyaaaaaa! Shoga mji wa moto huu, unaweza kukoroga maji ya baridi ukajua ni chai!  Acha nijimwayemwaye, wee shangaa kama mkulima wa vitunguu…

Mahaba: Punguza Moto Wali Uive

HALOOOO eeeehhh shoga wanakwambia mjini raha jipe mwenyewe, hata kama mtu mzima nunua pampas kisha jikojolee, kwani bei gani! Unajifanya kuvaa viatu virefu wakati hata ndala ya msalani huna!  Shoga usiwe kama pipa lililokosa mfuniko…

Taa ya gari haifungwi chumbani

WAAREEEEE miye ndiye dokta nimeachiwa hospitali wagonjwa wote ruksa kutibiwa bure, kulala bure hata wakitaka ruhusa nawaruhusu! Unaloooo bibiyeeee ulidhani ukivaa lemba ndiyo heshima wakati hata wasio wema wanalivaa! Heee heeeiyaaaa! …

Unachukua nafasi yako kama mke?

NI juma lingine tulivu kabisa tunakutana kwenye ukurasa huu ambao unapata fursa ya kusoma dondoo mbalimbali zinazoweza kuyaboresha maisha yako. Nikusihi tu uendelee kuwa mdau wa makala ninazoandika maana ni zenye manufaa kwenye maisha…

Utamu wa chai sukari

BINADAMU bwaana hata ukiogelea watakwambia unawatimulia vumbi, paaaambeee shoga! We endelea kunishangaa Anti Naa badala ushangae mlango mkubwa unalindwa kwa kufuli dogo, heee heeeeiyaaaa!  Shoga umbeya huu unaweza kujikuta unakata kiu…