Trump Ashinda Urais wa Marekani, Clinton Akubali Matokeo
MAREKANI: Mgombea Urais wa Chama cha Republican, Donald Trump ameshinda kiti hicho. Trumpa ambaye mpaka sasa ana kura 288 huku Hillary Clinton akiwa na kura 218 za wajumbe kati ya kura zote 538.
Kwa mujibu wa Katiba ya Marekani, Mshindi wa urais alitakiwa kushinda angalau kura 270 kati ya hizo 538 lakini Bw. Trump amevuka na kufikisha kura 279 mpaka sasa.
Clinton akubali kushindwa
CNN na NBC wameripoti kwamba mgombea wa chama cha Democratic Hillary Clinton amempigia simu Donald Trump na kukubali kushindwa.
This team has so much to be proud of. Whatever happens tonight, thank you for everything. pic.twitter.com/x13iWOzILL
— Hillary Clinton (@HillaryClinton) November 9, 2016
Shangwe kambi ya Trump
Shangwe, nderemo na vifijo zimetanda miongoni mwa wafuasi wa Donald Trump.
Trump: Asanteni sana
Trump amepanda jukwaani Manhattan, New York. Amewashukuru wafuasi wake na kusema amepigiwa simu na Hillary Clinton “kuwapongeza”.
Akizungumza na wafuasi wake baada ya kutangazwa mshindi, Trump amewataka raia wote wa Marekani, waliomchagua na ambao hawakumchagua kuungana na kuanza kuijenga nchi yao kwani muda wa kampeni na siasa za kugawanyika umekwisha.
Such a beautiful and important evening! The forgotten man and woman will never be forgotten again. We will all come together as never before
— Donald J. Trump (@realDonaldTrump) November 9, 2016
Comments are closed.