Michael Ray Stevenson ‘Tyga’ na Kylie Jenner.
Mwanamuziki Michael Ray Stevenson ‘Tyga’, amefunguka kuwa amewahi kuonywa kutoingia kwenye uhusiano wa kimapenzi na Mwanamitindo Kylie Jenner lakini cha ajabu hakuambiwa sababu za kuwa mbali na mwanamke huyo hivyo akapotezea.
Akizungumza na Jarida la Complex, Tyga alisema yeye alikuwa na mapenzi ya dhati na mwanamke huyo lakini kila alipokutana na marafiki zake walimtahadharisha kuwa mbali naye.
“Marafiki zangu wengi walikuwa wakinitahadharisha kuwa mbali na Kylie bila kunipa sababu, nilishindwa kuwasikiliza kwani moyoni nilimpenda sana,” alisema Tyga.
Comments are closed.