Uganda Yasitisha Kampeni za Uchaguzi Mkuu
SERIKALI ya Uganda imesitisha kampeni zote za uchaguzi wa Urais katika mji mkuu wa nchi hiyo Kampala na wilaya nyingine 10 zenye idadi kubwa ya watu.
Msemaji wa Tume ya Uchaguzi, Paul Bukenya, amesema sababu ya kufuta kampeni hizo ni ongezeko la maambukizo ya virusi vya Corona huku wakosoaji wakidai sababu halisi ni umaarufu wa upinzani katika maeneo hayo.
Taifa hilo limepanga kufanya uchaguzi wake mkuu Januari 14, 2021.