The House of Favourite Newspapers

Wanajeshi Waichapa Yanga

0

Timu ya Yanga imefungwa bao 1-0 katika mechi ya kirafiki jioni ya leo ilipocheza dhidi ya Ruvu Shooting kwenye Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, Dar es Salaam.

Katika mchezo huo, beki Abdallah Haji ‘Ninja’ alijifunga wakati alngoni akiwa kipa Ramadhan Kabwili katika dakika ya 22 alipokuwa akijaribu kuokoa krosi ya Shalla Juma kutoka upande wa kushoto wa Uwanja kuipatia bao pekee la ushindi Ruvu.

Huo ulikuwa mchezo wa pili wa kujipima nguvu kwa Yanga inayofundishwa na kocha Mzambia, George Lwandamina baada ya Jumamosi iliyopita kushinda 3-2 dhidi yas Singida United Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Kikosi cha Yanga kilikuwa; Ramadhani Kabwili, Hassn Kessy/Juma Abdul, Gardiel Michael, Abdallah Hajji ‘Ninja’, Vincent Andrew/ISSAMnigeria, Said Juma ‘Makapu’/Maka Edward, Pius Buswita/Said Mussa, Thabani Kamusoko, Donald Ngoma, Ibrahim Hajib/Raphael Daudi na Emmanuel Martin.

Ruvu Shooting; Bidii Hussein/Abdallah Rashid, Said Madega/Abdallah Mpambika, Yussuf Nguya, Frank Msese, Mangasini Mbonosi, Baraka Mtuwi/Chande Magoja, Jamal Soud/William Patrick, Shaaban Msala, Shalla Juma/Issa Kanduru, Fully Maganga na Khamis Mcha ‘Vialli’.

VIDEO YA MATOKEO YA UCHAGUZI MKUU WA TFF

Leave A Reply