The House of Favourite Newspapers

Wanaume Wamnyoosha Nisha

Salma Jabu ‘Nisha’

MSANII wa maigizo na vichekesho Bongo, Salma Jabu ‘Nisha’ amesema kuwa, amekoma kutoa mapenzi yake kwa wanaume wa Kitanzania kwa kuwa wote wana mapenzi ya kuigiza ambayo yamempotezea muda mno.

 

Akizungumza na Ubuyu, Nisha alisema ameumizwa sana na mapenzi ya Kibongo, hivyo bora kama anataka kuwa na mpenzi ni afadhali atafute mwanaume wa nje na si Mbongo tena.

 

“Hivi sasa hivi naanzaje kutoka kimapenzi na mwanaume wa Bongo walivyo waongo na walaghai maana nimepoteza muda mwingi kwao lakini hakuna chochote nilichopata zaidi ya fedhea tu,” alisema Nisha ambaye amewahi kutoka na staa wa Bongo Fleva, Nay wa Mitego.

Comments are closed.