Washindi ‘Toka na Mike’ Wapatikana Dar Live, Walamba Ajira (Picha + Video)
KINYANG’ANYIRO cha kutafuta watangazaji bora kilichofanyika katika Ukumbi wa Taifa wa Burudani wa Dar Live ulioko Mbagala-Zakhem, jijini Dar es Salaam, kiliisha kwa kuwaibua washindi watatu ambao waliingia mkataba wa kudumu wa kuitumikia Radio Times FM, ambao ni: Ramadhani Tembo wa Dar, Amina Bilia wa Mbeya na Geofrey Pangapanga.
Washindi hao walitangazwa na Katibu Mkuu wa Baraza la Sanaa (Basata) Geofrey Mungereza, aliyekuwa mgeni rasmi.
Baada ya watangazaji hao wapya kujitwalia ajira hizo Khadija Kopa, Barnabas na wasanii wengine waliendeleza burudani mpaka majogoo.
HABARI/PICHA: RICHARD BUKOS / GPL
Comments are closed.