Tinampay Amtisha Pialali, Naye Aapa Kumbomoa kwa KO – Video
ARNEL Tinampay bondia Mfilipino aliyeko nchini sasa amesema atamtwanga Pialali mapema kwa sababu ameshamsoma anacheza kama bondia Mtanzania, Hassan Mwakinyo, hivyo kwake yeye kazi itakuwa nyepesi tu kumtwanga mpinzani wake huyo Mtanzania mapema.
Naye Pialali anasema yeye na Mwakinyo ni mabondia tofauti na hawezi kufananishwa na bondia yeyote hapa nchini kwani ana uzoefu mkubwa na mashindano mengi makubwa ya kimataifa, uwezo wake na mbinu za mwalimu wake, hivyo Mfillipino huyo asijidanganye, atamtwanga kwa KO kwani hatorudi tena Tanzania.
Shughuli itakuwa pevu pale Next door Masaki jijini Dar es Salaam ambako tayari tikezi za pambano zinauzwa kwa kiingilio cha sh 20,000 mzunguko, Sh 50,000 kawaida na Sh 100,000 kwa VIP.
Tiketi hizo zinapatikana kupitia Nilipe App,Selcom,Vunja Bei Store na Vunja Bei Toto Sinza, Shishi Food Kinondoni, Cake City Njiapanda ya SalaSala, Kaites Lounge Tabata na Dick Sound Magomeni.
Pambano hilo limedhaminiwa na Gazeti jipya na bora la michezo nchini…. #SpotiXtraJumanne
Pamoja na: @255globalradio