The House of Favourite Newspapers

Yanga Yatamba Kuipiga Mtibwa

0
Kikosi cha timu ya Yanga.

YANGA leo inacheza na Mtibwa Sugar katika Ligi Kuu Bara kwenye Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam, lakini imetamba kushinda.

Wakati Mtibwa ikiwa kileleni, Yanga yenyewe ipo nafasi ya sita ikiwa na pointi nane, lakini kocha msaidizi wa timu hiyo, Shadrack Nsajigwa amesema kuwa wamejiandaa kushinda mchezo huo.

Nsajigwa alisema wanataka kushinda mchezo huo ili kujiweka katika mazingira mazuri ya kutetea ubingwa wao.

Akizungumza na Championi Jumamosi, Nsajigwa alisema wanajua Mtibwa ni timu nzuri iliyojiandaa kwa ushindani msimu huu lakini watakabiliana nayo ili kuhakikisha wanapata ushindi.

“Tumejiandaa vizuri kwa ajili ya kuhakikisha tunapata matokeo mazuri katika mechi yetu na Mtibwa japokuwa naamini itakuwa na ushindani mkubwa kwani wapinzani wetu wapo vizuri msimu huu.

“Katika mechi hiyo tutamkosa Tshishimbi (Papy Kabamba ana kadi tatu za njano) lakini nafasi yake kuna mchezaji ambaye tayari tumemwandaa kwa ajili ya kuiziba hivyo ni matumaini yetu kuwa tutafanya vizuri,” alisema Nsajigwa.

Kwa upande wake, Kocha wa Mtibwa, Zuberi Katwila amesema moto walioanza nao msimu huu ndiyo huohuo watakaoendelea nao leo dhidi ya Yanga.

“Tunaiheshimu Yanga lakini kwa sasa sisi ni bora kuliko wao na ndiyo maana tunaongoza ligi kwa hiyo tumejipanga kuhakikisha tunaibuka na ushindi,” alisema Katwila.

Leave A Reply