NAHODHA msaidizi na beki wa kati tegemeo wa Yanga, Kelvin Yondani amesema wanataka kuwashangaza mashabiki wao kwa kuweka bonge la rekodi dhidi ya Township Rollers ya Botswana.
Yanga, leo inatarajiwa kujitupa kwenye Uwanja wa Taifa wa Gaborone, Botswana kucheza na Rollers mechi ya Ligi ya Mabingwa Afrika.
Timu hizo zinavaana katika mechi ya marudiano ya raundi ya kwanza ya michuano hiyo baada ya mchezo uliopita Yanga kufungwa mabao 2-1 kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
Akizungumza na Championi Jumamosi kutoka Botswana, Yondani alisema katika mechi hiyo watapambana kufa au kupona kuhakikisha wanapata matokeo mazuri ya ushindi yatakayowavusha katika hatua inayofuata.
Yondani alisema, wana historia nzuri ya kupata matokeo mazuri ugenini kutokana na kucheza bila ya presha kama wanavyocheza mechi za nyumbani, hivyo ana matumaini ya kupata ushindi .
“Kikubwa tunataka kutengeneza historia ya kuwatoa Waswana ili tuwashangaze watu kwa sababu kila mtu anaamini kuwa tayari Yanga tumetolewa,” alisema Yondani na kuendelea.
“Kama umekuwa ukiifuatilia Yanga kwa ukaribu katika mechi za ugenini tumekuwa tukicheza kwa kiwango cha juu na kupata matokeo mazuri tofauti tukiwa nyumbani.
“Kwa upande wangu nimepanga kutimiza majukumu yangu vizuri pamoja na mabeki wenzangu kuhakikisha tunaokoa na kupunguza hatari langoni kwetu ili kuhakikisha haturuhusu bao.
Stori na Wilbert Molandi, Dar es Salaam
Comments are closed.