The House of Favourite Newspapers

EPL, LIGUE 1, COPPA ITALIA ZINAPIGWA ZA KIBABE LEO

0

Kunako ligi kuu ya Uingereza, ligi kuu ya Ufaransa na michuano ya Coppa Italia hatua ya nusu fainali kutakua na michezo mikali ya kukata na shoka ambayo itakwenda kurindima usiku wa leo.

Michezo kweli itapigwa mikali katika nchi hizo tatu usiku wa leo lakini mchezo ambao utakwenda kuvuta hisia za wapenzi wengi wa mpira wa miguu ni derby ya Merseyside katika ya klabu ya Everton ambao watakua wenyeji dhidi ya ya klabu ya Liverpool.

EPL

Moja ya michezo mikali inayosubiriwa leo ni mchezo mkali kati ya Everton na klabu ya Liverpool ambapo huu ni mchezo wa Derby, Mchezo huu licha ya kua derby lakini unakua mkali zaidi kwakua Liverpool wanahitaji ushindi katika kuwania ubingwa wa ligi kuu ya Uingereza lakini upande wa Everton wao wanapambania kutoshuka daraja.

Suka mkeka wako kwenye michezo mikali itakayopigwa leo kwenye michuano mbalimbali barani ulaya na duniani kote. Machaguo zaidi za 1000 yapo huku lakini vile vile Turbo Cash pia ipo. Unasubiri nini sasa? Ingia meridianbet na ubashiri sasa.`

Man United wao baada ya kutoka suluhu katika mchezo wa ligi kuu ya Uingereza dhidi ya Bournamouth wiki mbili zilizopita leo watakua nyumbani kumenyana na klabu ya Sheffield United inayoshika mkia kwenye ligi hiyo.

Mchezo mwingine mkali utakua baina ya klabu ya Crystal Palace ambao wametoka kuwapa kipigo kizito Westham United wikiendi iliyomalizika dhidi ya Newcastle United, Mchezo huu unatarajiwa kua mkali vilevile kwakua vilabu vyote vimekua kwenye kiwango kizuri kwenye michezo kadhaa iliyiopita.

LIGUE 1

Pale kwenye ligi kuu ya Ufaransa Ligue 1 mabingwa watetezi klabu ya PSG watakua ugenini kumenyama na klabu ya Lorient, Olympique Marseille watakua nyumbani kumenyana na OGC Nice, Mchezo mwingine utakua kati ya Monaco na klabu ya Lille ambapo ni moja ya michezo mikali kwenye ligi hiyo usiku wa leo.

COPPA ITALIA

Pale nchini Italia leo itapigwa nusu fainali ya marudiano ambapo klabu ya Atalanta watakua nyumbani kuikaribisha klabu ya Fiorentina ambao walishinda mchezo wa kwanza wakiwa kwao, Hivo mchezo wa leo ndo utaamua ni timu gani itacheza fainali ya michuano hiyo msimu huu ambapo watamenyana na Juventus ambao tayari wametangulia fainali baada ya kuitupa nje klabu ya Lazio usiku wa jana.

Leave A Reply