The House of Favourite Newspapers

MZEE AKILIMALI: NAGOMBEA URAIS YANGA, NIKISHINDA HAKUNA KULIA NJAA

Mzee Akilimali.

 

HAKUNA asiyemfaha­mu Mzee Akilimali kuto­kana na umaarufu wake ndani ya Klabu ya Yanga ambako amekuwa akivutana na baadhi ya wanachama wa klabu hiyo huku wakidai kuwa ndiyo anakwamisha maendeleo ya klabu.

 

Jina lake halisi ni Ibrahim Akilima­li. Huyo ni Katibu wa Baraza la Wa­zee la Yanga ambaye amekuwa akitoa maneno ya shombo kwa wachezaji au hata viongozi wa timu hiyo anapoona hawafanyi vizuri. Siyo kwamba haipendi Yanga, bali huyu ni Yanga lialia.

Kikosi cha timu ya Yanga.

Lakini wapenzi wa soka nchini wamekuwa waki­jiuliza mambo kadhaa kuhusi­ana na mzee huyo ambaye haishiwi vituko kila kukicha kama.

Cham­pioni lime­fanya naye mahojiano maalum ili kujua mambo kadhaa muhimu kuhusi­ana na Klabu y a Yan­ga.

 

LIGI IMEMALIZIKA NA YANGA IMESHIKA NAFASI YA TATU, UNASEMAJE?

“Lazima turidhike na yaliyotokea kwa sababu asiyekubali kushindwa siyo mshindani na siku zote mch­ezo wa mpira ni kama mchezo wa kupokezana kijiti.

 

“Naridhika na matokeo yaliyo­tokea katika mchezo japo hataku­wa vizuri, hata hivyo, niwashukuru wachezaji na viongozi wetu kwani hapa tulipofikia si pabaya zaidi, tu­ridhike, lakini tukumbuke mwisho wa ligi ndiyo mwanzo wa ligi.

 

“Haya yaliyotokea katika msimu mzima yawe funzo ya kuona tuliko­sea wapi ili msimu ujao tusirudie tena makosa yaleyale, ni lazima tu­jiimarishe ili tuweze kuirejesha Yan­ga katika nafasi yake ya kimataifa.

UNADHANI YANGA ILIKOSEA WAPI MSIMU HUU?

“Kiukweli Yanga ilikosea sehemu nyingi tu na zipo dhahiri, sehemu ya kwanza kulikuwa na tofauti kwa viongozi na wakati huohuo aliyekuwa mwenyekiti wetu, Yusuf Manji alijiuzulu, mambo ya kipesa yalikwenda ndivyo sivyo kwa hiyo tukikosea sehemu nyingi.

 

“Unafahamu wachezaji ni sawa na watoto ambao hawawezi waka­jua kwamba leo baba hana kitu maana siku zote wanafurahi kuona chungu kinachemka na wao wa­napata chakula, sasa kwa viongozi wetu ambao wapo hadi leo wal­ishindwa ile hekima ya kizee ya ku­jua wafanye nini ili watoto wapate chakula kama kawaida.

 

“Viongozi waliposhindwa hilo, wakawa wanapiga kelele kwamba hakuna pesa, mara Mzee Akilimali zile pesa ulizotuahidi zipo wapi, wale wafadhili wapo wapi? Jamani hivi ni kweli mimi Mzee Akilimali niliahidi wafadhili nitawaleta Yan­ga? Hamnisaidii hata nyinyi waandi­shi wa habari au niliwaahidi mimi ninazo pesa za kuwapa Yanga?

 

“Mimi nilikataa jamani uende­shaji wa klabu badala ya kuitwa Yanga Afrika iitwe Yanga Yetu, hi­cho ndicho nilichokataa, sikukataa labda kama ninawafadhili au nita­waleta kina nani, hapana, tusisingi­ziane, nilikataa Yanga kukodishwa ila sikusema hayo yaliyosemwa.

“Narudia tena, nilisema kwamba Yanga hii haikodishwi na hatuna sababu ya kupoteza, tathmini ya wazee wetu ambao ni waanzilishi wa Yanga Afrika, leo tuitoe huko tukaiite Yanga Yetu, hilo haliweze­kani, wakaniuliza labda mimi sitaki maendeleo ya Yanga, kiukweli mimi nataka maendeleo.

 

“Mimi ni mhanga wa maende­leo kwa sababu nakumbuka nim­etembea nusu ya Tanzania kwa lengo la kutaka Yanga ianzishe kampuni itakayojulikana Yanga Afrika Sports Cooperation Limited, iwe kampuni ya hisa tena itakuwa ya umma na kwa upande wa hisa klabu ibaki na asilimia 51 na wana­hisa wawe na asilimia 49.

 

WEWE NDIYO SABABU YA MANJI KUONDOKA NDANI YA YANGA?

“Wanasema kuyumba kwa Yan­ga, Mzee Akilimali ndiyo chanzo mpaka Manji kuachia ngazi kwa sababu nilikataa Yanga isikodish­we wala hakuna jingine ambalo nilikataa na mimi na Manji tulipata kukaa hivi nikamueleza baba una­potupeleka wapi, kwa nini hurudi nyuma.

 

“Na kilichomuondoa Manji Yan­ga lazima niwaambie Watanzania, siyo Mzee Akilimali, Akilimali mimi nani kwanza, hivi mende anaweza kuangusha kabati? Mimi sina hela, mimi ni lofa, hata hapa ninapokaa barabarani naonekana sina kitu, yaani mimi naweza kumpindua Manji kwa kipi labda.

 

“Ki l ichompindua Manji ali­kuwa hap­endi kush­irikiana na w e n z a k e w a k a w a sawa, ameji­uzulu baada ya SportPesa walipokubaliwa na uongozi wa Yanga kuwa wadhami­ni wa timu na siyo kwa sababu ya Mzee Akilimali.

UNAWEZA KUSEMA KIPINDI CHA MANJI KULIKUWA NA MATATIZO KAMA HAYA?

“Kuhusu suala la mishahara hata wakati wake watu walikaa hadi miezi miwili hawajalipwa kitu lakini kulikuwa na mtu anadhamini kila kitu na aibu hiyo ilikuwa haitoki.

“Lakini kulikuwa na udhamini na kulikuwa na mtu wa utunzaji wa pesa, hivi leo tuseme Yanga ni masikini kiasi hicho, Yanga siyo masikini, tuna Sportpesa wanatoa mamilioni mangapi, tuna watu sasa hivi wamekuja kuingia mikataba na Yanga kwa ajili ya kuuza jezi na wamesema watatoa bilioni sijui ngapi, sasa mipango ipo wapi.

 

WANADAI HALI YENU MBAYA INAZIDI KILA KUKICHA

“Hao kwa Yanga hii au nyingine, sisi tunachosubiri sasa hivi ni ku­ruhusiwa kufanya uchaguzi wetu na tukishafanya uchaguzi tu, Yanga itawekwa sawasawa, itakuwa klabu inayotisha Tanzania na Bara la Af­rika kwa sababu mipango itaku­wepo.

 

“Hawa viongozi wetu w a liokuwepo sasa mipango yao imefeli, walikuwa hawawezi kufanya mipango kwa kuwa walikuwa wategemezi lakini hao tutakaowachagua tuta­waambia dira yetu ndiyo hiyo, ipelekeni Yanga na wao wa­takuwa hawana tegemezi na watafanya mipango thabiti ya kuipeleka Yanga mbele.

 

Unasema mambo ya uch­aguzi, lakini uongozi ume­tangaza mkutano mkuu, hapa vipi?

“Wanapingana na serikali, serikali imewaambia hawataki mikutano isipokuwa wafanye uchaguzi ila wao wanasema hawatafanya hivyo.

 

UNATAKA UCHAGUZI, UNA MPANGO WA KUGOMBEA?

“Kama kweli uchaguzi uta­fanyika safari hii basi Mzee Ak­ilimali atakuwa Rais wa Yanga, hivyo lazima nigombee, nikiwa rais hakuna atakayelia njaa Yanga.

 

LAKINI SIYO MARA YA KWANZA KUSEMA HIVYO

“Wakati ule nilikuwa nime­muachia Manji lakini safari hii naingia mimi mwenyewe hakuna hata mchezaji wangu ambaye atapiga kelele kuhusu kulalamikia kuchelew­eshewa pesa zake.

 

LAKINI MWANZONI ULISEMA WEWE NI LOFA?

“Nasema hivi ukisikia mbwa anabweka basi ujue yupo kwao au nyuma yupo bwana wake au nikwambie, siwezi kuongea hilo, lakini ki­kubwa tuijenge Yanga yetu kutokana na haya tuliyoyavu­na ndani ya msimu huu.

“Naamini tukifanya hivyo kwenda katika uchaguzi hala­fu tukachagua viongozi wapya basi tutatisha msimu ujao na kurudisha heshima yetu.

 

YANGA INAKWENDA KUWA WA MCHANGANI MSIMU UJAO, UNAZUNGUMZIAJE?

“Tunakwenda kwenye msimu mpya sawa kwani hata Simba haikuweza kush­iriki michuano ya kimataifa kwa muda wa miaka mitatu mpaka tumewaita wazee wa mchangani unadhani wali­kuwa hawajipangi kwa ajili ya kuleta mafanikio.

 

“Basi na sisi tutajipanga na hatuwezi kuwa wa mchanga­ni kama walivyokuwa wao kwa sababu Simba haitoweza kuchukua ubingwa mara mbili mbele yangu nikiwa rais wa Yanga, hiyo mara moja itakuwa inamtosha kabisa na wakipanda ndege na sisi tu­napanda ndege.

 

UNAZUNGUMZIAJE DONALD NGOMA KUONDOKA?

“Ngoma muache aende tu kwa sababu hata msimu huu ameshindwa kuwa msaada katika timu kwa kuwa amecheza mechi nne pekee kati ya 30 za msimu mzima.

“Pia mkumbuke Ngoma wakati yupo kule FC Plati­num nilibahati kwenda kule waliweza kusema uwezo wake ndani ya uwanja na pia walitoa angalizo kuhusiana naye kuwa ni msumbufu na ni kweli yamekuja kutokea yale ambayo tuliambiwa kule na wakati ule sikuwa na uwezo wa kuongea na vion­gozi lakini ngojeni tufanye uchaguzi na mimi nitakuwa pale kama kiongozi.

 

“Na hao wachezaji wen­gine wa kimataifa wakitaka kuondoka waondoke wote tu, mfano, Chirwa (Obrey) amejiita mzee wa kulima ndi­yo akawa amepotea kabisa.

“Wameondoka wengi Yan­ga waache waende mbona Niyonzima (Haruna) ameon­doka.

 

VIPI KUHUSU KELVIN YONDANI?

“Kiukweli kama kweli Kel­vin Yondani ataondoka Yan­ga nitaumia na nitalia sana kwa sababu ni mmoja kati ya wachezaji ambao walikuwa wanacheza kwa kuji­tuma sana, ni bora waende wote ila yeye abaki pale Yanga na kipindi hiki ndiyo alitakiwa abaki kurithi mikoba ya Cannava­ro (Nadir Haroub) kuweza kuwaon­goza wen­zake.

Comments are closed.