The House of Favourite Newspapers

AIRTEL YATANGAZA WASHINDI PROMOSHENI YA AMSHA AMSHA

Meneja Uhusiano Airtel Tanzania, Jackson Mbando, akizungumza na waandishi wa habari wakati wa kutangaza washindi wa kwanza wa promosheni ya mwezi mmoja ya AMSHA AMSHA na Airtel Money na ushinde ambayo ilizinduliwa Juni 14 mwaka huu.
Meneja Uhusiano SportPesa, Sabrina Msuya akifafanua jambo.
…Akiwapigia simu washindi wa promosheni hiyo.

 

KAMPUNI ya simu za mkononi ya Airtel leo kwa kushirikiana na SportPesa imetangaza washindi wa kwanza wa promosheni ya mwezi mmoja ya AMSHA AMSHA na Airtel Money na ushinde ambayo ilizinduliwa Juni 14 mwaka huu.

 

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo wakati wa kutangaza washindi hao, Meneja Uhusiano Airtel Tanzania, Jackson Mbando, alisema kuwa droo ya kupata washindi hao imesimamiwa na kuchezesha kwa wazi na Bodi ya Michezo ya kubahatisha Tanzania ambayo ndio wenye jukumu la kusimamia michezo yote ya bahati nasibu hapa nchini.

 

Kama mlivyoona hapa kwa siku ya leo, droo yetu imechezesha kwa uwazi na hii inaamanisha kila mteja anayo fursa ya kuwa mshindi alisema Mmbando huku akiongeza kuwa kile mteja wa Airtel Money anachotakiwa kukifanya ni kuhakikisha anabet siku ambayo droo iko wazi na moja kwa moja namba yake itaingizwa kwenye droo ya wiki. ‘Mteja atatakiwa kubet siku ya droo ili kupata nafasi ya kuwa moja ya washindi, alisema Mmbando huku akiongeza kuwa wateja wanatakiwa kuhahakikisha kuwa wanayo pesa kwenye akaunti yao ya SportPesa.

 

Mmbando alisema kuwa washindi wa leo kumi wamejishindia simu mpya za smartphone kila mmoja, wengine kumi wamejishindia jezi za timu za Simba na Yanga huku wengine kumi kila mmoja akijishindia tiketi ya kushuhudia mechi za Simba na Yanga kwa msimu wote wa 2018/2019. Natoa rai kwa wateja wote wa Airtel kushiriki kwenye hii promosheni ya AMSHA AMSHA USHINDE NA AIRTEL MONEY kwani muda bado hupo na zawadi kwa washindi bado ni nyingi, alisema Mmbando huku akiongeza kuwa mshindi mmoja kwa siku ya leo amejishindia TV mpya yenye inchi 32 pamoja na ving’amuzi kutoka Star Times.

 

 

AMSHA AMSHA USHINDE NA AIRTEL MONEY inatoa nafasi kwa wateja wetu wa Airtel Money kuweza kujishindia zawadi kabambe kwa kubet kwa kutumia Airtel Money. ‘Airtel siku zote tunaleta huduma na bidhaa zenye ubunifu na za kutuweka karibu na wateja wetu. Tunaelewa ya kwamba michezo pamoja na mambo ya kubet imekuwa na maisha ya kawaida kwa wateja wetu. Kwa kuzindua promosheni hii ambayo tumeshirikiana na SportPesa inatoa nafasi nyingine ya kuendelea kutuweka karibu na wateja wetu’, aliongeza Mmbando.

 

Kwa upande wake, Meneja Uhusiano SportPesa Sabrina Msuya alisema kuwa tangu kuzinduliwa kwa promosheni ya AMSHA AMSHA USHINDE NA AIRTEL MONEY 14 Juni mwaka huu, droo imekuwa wazi kila siku kuanzia saa sita usiku mpaka 11:59 kwa siku inayofuata kwa muda wote wa promosheni na kila mteja anachotakiwa kufanya ni kubet siku ya droo na namba yake itaingizwa kwenye droo moja kwa moja.

 

Msuya alisema zawadi za kila siku ni simu mpya za smartphone, jezi za Simba na Yanga pamoja na tiketi za kushuhudia mechi za Simba na Yanga msimu wote huu huku za kila wiki ikiwa na TV mpya yenye inchi 32 pamoja na ving’amuzi kutoka Star Times.

 

 

Kile ambacho mteja anachotakiwa kufanya ni kujiandikisha, kuweka pesa kwenye akaunti yake ya SportPesa kwa kutumia Airtel Money halafu ndio abeti, alisema Msuya huku akiongeza kuwa washindi wanaweza kuchukua zawadi zao kutoka duka lolote la Airtel hapa nchini.

 

 

Comments are closed.