DULLAH MBABE AMTWANGA SAIDI MBELWA DAR LIVE
Dullah na wapambe akipanda ulingoni kabla ya pambano.
BONDIA wa kulipwa, Abdallah Pazi ‘Dullah Mbabe’, amefanikiwa kumchakaza vikali mpinzani wake, Saidi Mbelwa ‘Moto wa Gesi’. katika pambano la kumaliza ubishi lililofanyika jana usiku kwenye Ukumbi wa Dar Live, uliopo Mbagala Zakhem,jijini Dar es Salaam.
Katika pambano hilo ambalo lilikuwa la kumaliza ubishi kati ya mabondia ambapo Mbabe alifanikiwa kuongoza raundi nyingi licha ya kuumia bega la mkono wake wa kushoto lakini alifanikiwa kumuangusha mpinzani wake mara mbili katika raundi ya tatu na ya nne.
Kabla ya pambano hilo kubwa waliweza kushuhudia mapambano ya utangulizi huku lililovutia zaidi ni pambano la wadada kati ya Maimuna Hashimu na Happy Daudi ambalo lilimalizika kwa Happy Daudi kushinda kwa pointi .
Mapambano mengine ya utanguliza yalikuwa kati Paulo Kamata na Shabani Kaoneka na Paulo kamata akiibuka mshindihuku Saidi Wigo akipigwa na Faraji Sayuni kwa pointi.
PICHA NA RICHARD BUKOS | GPL
Comments are closed.