The House of Favourite Newspapers

Mnaokwenda Simba, Rudisheni Matumbo Yenu Nyuma

GUMZO la uchaguzi wa Simba limekuwa si kubwa sana, kwa kiasi fulani linaonekana kupun­guzwa na kasi ya masharti kutoka katika katiba mpya.

 

Uchaguzi mkuu wa Simba ambao umepangwa kucha­gua viongozi kwa mara ya kwanza chini ya mfumo mpya wa uwekezaji, utafanyika No­vemba 3, mwaka huu.

Sote tunajua, katiba mpya ya Simba imewabana baadhi ya viongozi wa klabu hiyo ku­shiriki.

 

Mambo mawili yamewaen­gua baadhi ya viongozi ku­shiriki. Elimu halafu suala la umri kwani inaonekana mwenye umri kuanzia miaka 65, haruhusiwi kushiriki.

 

Hii imewafanya baadhi yao kushindwa kuingia, hasa wale maarufu ambao tume­kuwa tukiwajua na waliku­wepo ndani ya Simba.

Lakini pia, suala la elimu, suala la shahada au digrii pia limekuwa kikwazo kwa wengi hasa waliotaka kuwania na­fasi ya mwenyekiti wa klabu hiyo.

 

Haya mambo mawili kwa kiasi kikubwa, yamesababi­sha ukimya na hali ya utulivu. Kama unakumbuka mwan­zoni ilikuwa ni vigumu kwa wengi kujitokeza.

Baada ya kelele za hapa na pale, baadhi wakaanza kuji­tokeza huku ikionekana bado kuna ugumu.

 

Kama mdau wa mpira Tan­zania na hasa kwa wale wa­naotaka kuona maendeleo, nilieleza wazi ambavyo ni­likuwa nikiamini itakuwa sa­hihi na hasa suala la kuhusi­ana na watu wengi kujitokeza na pia wajitokeze ambao watakuwa wamelenga ku­saidia maendeleo ya Klabu ya Simba.

 

Simba ambayo inakwenda katika mfumo mpya, kwani kuunda bodi ya wakurugenzi, itawakutanisha upande wa klabu na upande wa mweke­zaji. Lazima upande wa mwekezaji utakuwa na watu makini.

Hivyo ni lazima upande wa klabu nao uwe na watu ma­kini wanaoeleweka na wenye nia ya kuikomboa klabu hiyo badala ya matumbo yao au kuangalia mwekezaji pekee anataka nini.

 

Mjadala wangu wa leo un­aanzia hapo. Kwamba wakati wale wanaokwenda kuwania uongozi tunaamini ni watu imara, basi niwakumbushe tena kwamba wanapaswa ku­rudisha matumbo yao nyuma ili watangulize mioyo yenye nia njema ya kuisaidia Simba kubadilika na kupata maen­deleo zaidi, jambo ambalo limekuwa kilio cha milele.

 

Kilio cha maendeleo ki­naonekana kukosa namna njema kwa kuwa viongozi wengi wameingia kuongoza klabu wakiwa wamelenga zaidi kujisaidia au kujifaidi­sha wao.

Nataka nieleweke, sijas­ema waliopo sasa wanataka kujifaidisha. Ila wapo walio­wahi kujifaidisha na huenda wamerejea kwa kuwa wame­jirekebisha.

 

Sasa tunataka kuwakum­busha mapema kabisa kuhu­siana na hilo kuwa maen­deleo ya Simba yatapatikana kwa nia njema na wale wali­olenga kuisaidia klabu hiyo.

Kama wanaoingia kugo­mbea uchaguzi wa Simba na waliwahi kuongoza, halafu kukawa hakuna mafanikio. Naamini hawa ni wazuri na watakuwa wana jambo jipya wanataka kurudi nalo.

 

Lakini lazima tukubali, pamoja na hivyo nao wa­napaswa kujua Simba ni ya watu na wanapaswa kubadi­lika na watakapopata nafasi basi wafanye kile ambacho kinakusudiwa na wengi.

Haitakuwa sahihi kuwa na viongozi fuata mkumbo, vi­ongozi fuata upepo au vion­gozi walio tayari kutekeleza yale ambayo yanaweza ku­wafaidisha wao na watu wao.

 

Badala yake wawe viongozi imara, si kwa kupinga kila ki­takachotolewa na upande wa mwekezaji. Badala yake wale ambao wanataka Simba ien­delee na wao kubaki kwenye rekodi na historia kupitia ma­badiliko waliyoyafanya.

 

Simba haitapiga hatua kama wanaoiongoza nia yao haitakuwa njema. Kama Simba itashindwa kupata mafanikio katika mabadiliko ya sasa, hakuna maana ya mabadiliko hayo, na hakuna klabu itaona kuwa mabadi­liko yana manufaa.

 

Kuna kila sababu ya kulio­na hili mapema na kama wewe ni kiongozi unaona unataka kutanguliza tumbo, basi mapema ukae kando. Kama unaona nia yako ni ku­jifaidisha, imetosha. Waachie wenye nia nzuri na wewe un­aweza kufanya mambo yako mengine.

Comments are closed.