The House of Favourite Newspapers

Zahera Amkimbiza Kiungo Yanga

Msham­buliaji wa Yan­ga, Emmanuel Martin.

KIUNGO msham­buliaji wa Yan­ga, Emmanuel Martin ameondoka kwenye timu hiyo na kwenda kujiunga na Ruvu Shooting katika usajili huu wa dirisha dogo la usajili.

 

Hiyo, ikiwa ni siku mbili zimebaki kabla ya usajili wa dirisha dogo kufungwa na Shirikisho la Soka Tanza­nia (TFF).

Martin ali­jiunga na Yanga katika msimu wa 2016/2017 akitokea JKU inayo­shiriki Ligi Kuu ya Zan­zibar akisaini mkataba wa miaka miwili.

 

Kwa mujibu wa taar­ifa ambazo imezipata Championi Ijumaa, kiungo huyo mkataba wake umemalizika tangu mwezi No­vemba kabla ya uongozi kusitisha mpango wa ku­muongezea mkataba mwingine.

 

Mtoa taarifa huyo alisema sababu iliyo­sababisha kiungo huyo kutoongezewa mkataba ni baada ya kushindwa kumshawi­shi kocha mkuu wa timu hiyo Mkon­goman, Mwinyi Zahera.

“Martin rasmi siyo mchezaji wa Yanga na tayari amesaini mkataba wa mwaka mmoja wa kuichezea Ruvu Shooting baada ya kufikia makubaliano ya kuondoka Jang­wani.

 

“Anaondoka Yanga baada ya mkataba wake kumalizika na viongozi kusi­tisha mpango wa kumuongezea mwingine kutokana na kocha kutooneka­na kumhitaji.

 

“Kabla ya kuon­doka, Martin aliulizia hatma yake kwa viongozi wa Yanga akaona kimya, hivyo katika kujinusuru akaona aondoke zake Ruvu,” alisema mtoa taarifa huyo.

 

Alipotafutwa Mar­tin kuzungumzia hilo alisema: “Nipo katika hatua za mwisho za kukamilisha usajili wangu huku Ruvu Shooting ni baada ya kuona viongozi wa Yanga wapo kimya.

 

“Nikiri mkataba wangu kumalizika, hivyo ninakwenda huko Ruvu kwa ajili ya kupata nafasi ya kucheza baada ya Yanga kutopata kwa muda mrefu, hivyo ninaamini nikiwa huku nitakirejesha kipaji changu,” al­isema Martin.

STORI: Wilbert Molandi

Comments are closed.