The House of Favourite Newspapers

‘African Women And Beyond’  Kuwawezesha Wanawake Wa Tanzania

1.Baadhi ya akina mama waliojiunga na taasisi hiyo wakishiriki katika uzinduzi huo.Baadhi ya akina mama waliojiunga na taasisi hiyo pamoja na waanzilishi wa taasisi husika wakishiriki katika uzinduzi huo.2.Mapaparazi wakichukua tukio hilo.Mapaparazi wakichukua matukio katika hafla hiyo.3.Mwanzilishi wa taasisi hiyo,Joe Kariuki (kulia) akikata utepe kuashiria uzinduzi wa asasi hiyo hapa nchini TanzaniaMwanzilishi wa taasisi hiyo, Joe Kariuki (kulia) akikata utepe kuashiria uzinduzi wa taasisi hiyo nchini Tanzania4.Waanzilishi wa taasisi hiyo,Maetine Kappel (kushoto) na Joe Kariuki.Waanzilishi wa taasisi hiyo, Maetine Kappel (kushoto) na Joe Kariuki.5.Mmoja wa akina mama wa kitanzania,Jyot Ajay Ladwa (katikati) akijisajili kwenye fomu maalum.Mmoja wa akina mama wa Tanzania, Jyot Ajay Ladwa (katikati) akijisajili.

TAASISI  ya African Women and Beyond imepanga kuwawezesha wanawake wa Tanzania kwa kuwapatia mikopo nafuu na mafunzo ya biashara ndogondogo.

Akizungumza wakati wa hafla ya uzinduzi wa taasisi hiyo jana jijini Dar es Salaam, mwanzilishi wa taasisi hiyo, Joe Kariuki, alisema  taasisi hiyo ilianzishwa mwanzoni mwa mwaka huu nchini Kenya ikiwa na lengo la kuwawezesha akina mama wafanyabiashara ndogondogo na wakubwa kuwainua kiuchumi kwa kuwapa mafunzo na mbinu za kufanya biashara.

Kariuki alisema,   wanawake zaidi ya 4,000 nchini Kenya wamefanikiwa kujiunga na taasisi hiyo na tayari wanaendelea kupata mafunzo na elimu juu ya uendeshaji wa mitaji yao.

Aliongeza kwamba sasa Watanzania wanayo nafasi ya  kuwezeshwa kujiunga na  taasisi hiyo.

“Wananchi  hapa nchini ambao watakuwa wamejiunga kwa kujaza fomu maalum wataungana na Wakenya  mwezi Machi 2016 kwa ajili ya kupewa mafunzo ya  kufahamiana kwa kujenga uhusiano mwema miongoni mwao,” alisema.

NA DENIS MTIAMA/GPL

Comments are closed.