The House of Favourite Newspapers

Airtel: Taarifa kwa Umma Kuhusu Uzimaji wa Simu Bandia

1

airtel-new-logo-verTAARIFA KWA UMMA

Kufuatia kutimiza agizo la uzimaji wa simu bandia, kutokana na agizo elekezi la Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania TCRA.

Kampuni ya simu za mkononi ya Airtel inapenda kuwajulisha wateja wake walio nunua simu orijino kutoka kwa watoa huduma ndani ya maduka yetu ya Airtel, endapo baadhi ya wateja simu zao zitazima kutokana na agizo hilo. Airtel inawatangazia wateja wote watakaoathirika na zoezi hili kutembelea maduka yetu nchi nzima kwaajili ya kuhudumiwa/kurekebishiwa simu zao wakiwa na simu husika pamoja na risiti za manunuzi ya simu hizo.

Tunaomba radhi kwa usumbufu wowote utakaojitokeza kutokana na zoezi hili.

Imetolewa na Idara ya mawasiliano Airtel Tanzania

1 Comment
  1. Nsolo S. Stephen says

    Kwa aliyepoteza risiti inakuwaje?

Leave A Reply