KOCHA wa zamani wa Manchester United, Sir Alex Ferguson ameelezea mabadiliko ya aliyekuwa kiungo wake David Beckham kabla na baada ya kumuoa Victoria ambaye ni msanii wa muziki.
Ferguson anasema: “Hakuwa tatizo hadi alipooa. Alikuwa akiingia kazini na makocha wa akademi wakati wa usiku, alikuwa kijana mzuri sana.
“Kuoa katika eneo hilo la burudani lilikuwa jambo baya – kutoka wakati huo, maisha yake hayakuwa kama mwanzo. Ni mtu mashuhuri sana, soka ni sehemu ndogo tu.”
TAKWIMU ZA BECKHAM UNITED:
Michezo 387
Mabao 85
Asisti 98
Vikombe 10