The House of Favourite Newspapers

Alikiba Apata Shavu la Kushirikiana na Msanii Mkubwa Nigeria

 

MSANII kutoka Nigeria, Enitimi Alfred Odom maarufu kama ‘Timaya’, amempa shavu msanii wa Tanzania, Alikiba, kwenye EP  yake ya ‘Chulo Vibes’ ambayo inategemewa kuingia sokoni ndani ya mwaka huu.

 

Timaya amethibitisha taarifa hizo kupitia akaunti yake ya Instagram kwa kuandika, “My BROTHER @officialalikiba from TANZANIA came through on the EP. CHULO VIBES is 🔥🔥🔥”

 

Alikiba anafanya vizuri mpaka wakati huu na wimbo wake wa ‘Kadogo’ ambao una watazamaji zaidi ya milioni mbili kwenye mtandao wa Youtube.

Comments are closed.