Amber Lulu, Makomando Wafunika Usiku wa Miss Kinondoni 2019 – Video
USIKU wa kuamkia Julai 13, 2019, wasanii wa Bongo Fleva, Lulu Euggen ‘Amber Lulu’, Kundi la Makomando, Bi. Aisha na Wine walitoa shoo ya aina yake usiku wa kumtafuta Miss Kinondoni katika ukumbi wa Life Park Mwenge, ambapo mlimbwende Queen Mugesi Aynory (19) ameibuka kidedea na kuvaa taji lililokuwa linashikiliwa na Queen Elizabeth Makune.
Mshindi wa pili alikuwa Prisca Kisunda, wa tatu Leila Adim, wa nne Queen Anthony na wa tano Flaviana Sreven.
Comments are closed.