The House of Favourite Newspapers

Athumani Nyamlani Atangaza Kujitoa Kuwania Urais Tff

0

Makamu wa Rais wa zamani wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Athumani Nyamlani amejitoa kwenye kinyang’anyiro cha kuwania urais wa shirikisho hilo unaotarajiwa kufanyika Agosti 12, mwaka huu.

Nyamlani aliwasilisha barua TFF leo Jumapili Juni 25, mwaka huu ikiwa ni siku moja tu tangu Kamati ya Uchaguzi ipitishe jina lake kuwa miongoni mwa wagombea 10 wanaowania nafasi hiyo ya urais. Sababu aliyoeleza ni masuala binafsi.

Kwa msingi huo, wagombea wanaobaki kwenye kinyang’anyiro na kuhitajika kufika kwenye usaili kuanzia Juni 29, mwaka huu ni tisa wakiongozwa na Rais wa sasa, Jamal Malinzi anayetetea nafasi.

Mbali ya Malinzi wengine wanaowania nafasi hiyo ni Imani Madega, Wallace Karia, Fredrick Masolwa, Fredrick Mwakalebela, John Kijumbe, Shija Richard, Ally Mayay na Emmanuel Kimbe.

Waliojitokeza kuwania Makamu wa Rais na kurejesha fomu wako Mulamu Ng’hambi, Michael Wambura, Geofrey Nyange, Mtemi Ramadhani, Robert Selasela na Stephen Mwakibolwa.

Mbali ya nafasi za urais na makamu rais, Abdallah Mussa – aliyekuwa akiwania nafasi ya kugombea ujumbe wa Kamati ya Utendaji TFF kutoka Kanda Na. 1 (Mikoa ya Kagera na Geita) aliondolewa kwa sababu ya kutoambatanisha kivuli cha cheti ya elimu ya sekondari.

Hivyo wagombea wa nafasi za Wajumbe wa Kamati ya Utendaji kwa kufuata Kanda 13 ni kama ifuatavyo:

Kanda Na. 1 Mikoa ya Kagera na Geita;

Soloum Chama

Kaliro Samson

Leopold Mukebezi

Kanda Na. 2 Mikoa ya Mara na Mwanza;

Vedastus Lufano

Ephraim Majinge

Samwel Daniel

Aaron Nyanda

Kanda Na. 3 Mikoa ya Shinyanga na Simiyu;

Benista Rugora

Mbasha Matutu

Stanslaus Nyongo

Kanda Na. 4 Mikoa ya Arusha na Manyara;

Omari Walii

Sarah Chao

Peter Temu

Kanda Na. 5 Mikoa ya Kigoma na Tabora;

John Kadutu

Issa Bukuku

Abubakar Zebo

Francis Michael

 

Kanda Na. 6 Mikoa ya Katavi na Rukwa;

Kenneth Pesambili

Baraka Mazengo

Kanda Na. 7 Mikoa ya Mbeya, Songwe na Iringa;

Elias Mwanjala

Cyprian Kuyava

Erick Ambakisye

Abousuphyan Silliah

Kanda Na. 8 Mikoa ya Njombe na Ruvuma;

James Mhagama

Golden Sanga

Vicent Majili

Yono Kevela

 

Kanda Na. 9 Lindi na Mtwara;

Athuman Kambi

Dunstan Mkundi

 

Kanda Na. 10 Mikoa ya Dodoma na Singida;

Hussein Mwamba

Mohamed Aden

Musa Sima

Stewart Masima

Ally Suru

George Benedict

 

Kanda Na. 11 Mikoa ya Pwani na Morogoro;

Charles Mwakambaya

Gabriel Makwawe

Francis Ndulane

Hassan Othman ‘Hassanol’

Kanda ya 12. Mikoa ya Kilimanjaro na Tanga

Khalid Mohamed

Goodluck Moshi

Thabit Kandoro

Kanda Na. 13 Mkoa wa Dar es Salaam

Emmanuel Ashery

Ayoub Nyenzi

Saleh Alawi

Shaffih Dauda

Abdul Sauko

Peter Mhinzi

Ally Kamtande

Said Tully

Mussa Kisoky

Lameck Nyambaya

Ramadhani Nassib

Aziz Khalfan

Jamhuri Kihwelo

Saad Kawemba

Bakari Malima

Leave A Reply