The House of Favourite Newspapers

AUNT Acharuka Iyobo Kuitwa Dansa

MREMBO wa Bongo Movies, Aunt Ezekiel ameibuka na kuwacharukia wale wanaomchukulia baba watoto wake, Mozes Iyobo kama dansa wakati yeye anamuona kama mkurugenzi

Aunt alisema amekuwa akifuatilia kwenye mitandao ya kijamii na kuona watu wakimchukulia poa Iyobo lakini anawaambia tu, yeye kwake anamuona kama mkurugenzi.

“Waache kumchukulia poa Moze wangu. Mimi namuona kama mkurugenzi fulani hivi, wao wakiona mtuanacheza muziki hawajui kama ni kazi, hawathamini na kuonesha dharau tu mitandaoni,” alisema Aunt.

Comments are closed.