The House of Favourite Newspapers

Aunty Lulu Ampa Tano RPC wa Kikohozi

Aunty Lulu

BAADA ya hivi karibuni aliyekuwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Magharibi ambaye kwa sasa amehamishiwa Mkoa wa Kaskazini Pemba visiwani Zanzibar, RPC Hassan Nassir kutoa tamko la wanaume wanaokohoa wanawake wenye makalio makubwa wanapokatiza kuwa ni kosa kisheria, mwanadada kutoka Bongo Muvi, Lulu Semagongo ‘Aunty Lulu’ amempa tano kamanda huyo kwa hatua hiyo.

 

Related image

 

Akichonga na Za Motomoto News, Aunty Lulu alisema kuwa, anampongeza RPC Nassir kwa hatua hiyo kwa kuwa yeye ni miongoni mwa wanawake ambao wamekuwa wakikutana na kero kubwa kutokana na umbo lake kwani kila akikatiza kwenye kundi la wanaume, humpigia miluzi, kumzomea na kujikohoza hovyo hivyo sheria kwamba wanaofanya hivyo ni shambulio la aibu na kwamba watapandishwa mahakamani itasaidia kutokomeza tabia hiyo.

 

“Kiukweli ninampongeza sana Kamanda Nassir maana wanaume wamezidi, wamekuwa wakizomeazomea tu na kuguna kila mwanamke aliyefungashia anapopita mbele ya macho yao, sasa wakipandishwa mahakamani naamini watakuwa wanawaheshimu wanawake,” alisema Aunty Lulu.

 Stori: Gladness Mallya, Dar

Comments are closed.