Azam FC Yaipania URA Fainali Mapinduzi Cup
NAHODHA wa Azam FC, Himid Mao amefunguka kuwa anaamini watapata ushindi katika mchezo wa fainali ya Kombe la Mapinduzi dhidi ya URA, kesho Jumamosi kwenye Uwanja wa Amaan mjini Unguja.
Akizungumza na Championi Ijumaa, Mao alisema hadi kufikia fainali wamepambana na ni kitu kizuri lakini akasema safari hii wataongeza nguvu ili wakamilishe kazi kwa kutwaa ubingwa wa michuano hiyo.
Amesema kuwa wapinzani wao wana timu nzuri lakini watapambana nao, kauli ambayo iliungwa na mshambuliaji wa Azam FC, Shabani Iddi wa Azam FC ambaye alisema mbali na kujituma atatumia mchezo huo kuonyesha kuwa yupo fiti kwa ajili ya kucheza katika kikosi cha kwanza.
“Umeona nimerejea uwanjani lakini bado sijawa fiti kwa silimia zote, nashukuru kwa kupewa nafasi lakini tutapambana ili kuwa mabingwa,” alisema Idd.
Stori: Kazija Thabit, Unguja
Comments are closed.