Mkongwe wa Bongo, Haji Adam ‘Baba Haji’
Stori:Mwandishi Wetu, RISASI JUMAMOSI
MUIGIZAJI mkongwe Bongo, Haji Adam ‘Baba Haji’, amesema baada ya kucheza kwa mafanikio filamu ya Ndoto Bayana, ambayo ina maudhui ya dini ya Kikristo, sasa anakusudia kufanya kazi nyingine kama hiyo, lakini kwa Kiislamu.
“Nimejikuta nikipata wazo kuwa naweza nikafanya kazi hizi za kidini na bado nikawa nipo sokoni kama kawaida, kitu kingine kilichonivutia filamu hizi ni kuwa licha ya kutoa burudani kwa mashabiki, lakini pia zinafundisha sana. Nadhani ni muda muafaka wa kubadilika,” alisema.
Akiizungumzia filamu hiyo, Baba Haji alisema inazungumzia ndoto iliyokuwa ikiotwa na mkewe, ikiashiria ujio wa tukio la kishirikina, ambalo lilishindwa kutokana na nguvu ya maombi. Wengine walioshiriki filamu hiyo ni Thea, Patcho Mwamba na ‘mkewe’ Maureen Kunambi ‘Hakiki’.
KUNUNUA NA KUSOMA MAGAZETI YA GLOBAL PUBLISHERS ONLINE, INGIA HAPA==>VODACOM M-PAPER APP
*********
JIUNGE NA SOCIAL MEDIA ZETU
KWA HABARI ZA KITAIFA, KIMATAIFA, MASTAA NA MIKASA YA KUSISIMUA
INSTAGRAM: @Globalpublishers
ERIC SHIGONGO INSTAGRAM: @ericshigongo
TWITTER: @GlobalHabari
FACEBOOK: @GlobalPublishers
SUBSCRIBE YOU TUBE: Global TV Online
GLOBAL TV ONLINE: www.globaltvtz.com
HADITHI ZA KUSISIMUA NA MBINU ZA UJASIRIAMALI, ERIC SHIGONGO FACEBOOK PAGE:@shigongotz