BALOZI wa China nchini Tanzania, Wang Ke, leo amezindua ujenzi wa ofisi ya walimu katika shule ya sekondari ya Makumbusho na kuahidi kujenga ofisi nne za walimu za Mkoa wa Dar es Salaam ili kusaidia kuinua kiwango cha elimu ikiwa ni juhudi za kumuunga Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda.
Akizungumza katika uzinduzi huo, balozi huyo amesema nchi yake itaendelea kusaidia Tanzania katika shughuli za maendeleo hususani kujenga ofisi za walimu ili utoaji elimu bure kwa watoto wa Tanzania uende sambamba na mazingira mazuri ya walimu.
Naye Makonda amemshukuru balozi huyo akisema China imekuwa msatari wa mbele kwa kuiwezesha Tanzania katika mambo mbalimbali ya kimaendeleo na kuahidi kuendelea kuipa ushirikiano nchi hiyo kwa shughuli mbalimbali.
Aidha amewataka wananchi wa mkoa huo kuwapuuza viongozi wa kisiasa wanawaobeza wafadhili wanapotaka kujenga ofisi za walimu kwenye mkoa wake kwani waalimu ni watumishi wa umma na hawahusiani na masuala ya kisiasa.
NA DENIS MTIMA/GPL
Comments are closed.