BEKI Mtanzania, Abdi Banda, anayecheza soka la kulipwa nchini Afrika Kusini katika Klabu ya Baroka, alivutiwa na matayarisho na utengenezaji wa magazeti wa Global Publishers alipotembelea ofisi za Global Group zilizopo Sinza Mori jijini Dar hivi karibuni.
Akiongea na mtandao wa Global Publishers, mchezaji huyo alisema “nimevutiwa na jinsi wasanifu kurasa wa Global Publishers wanavyofanya kazi kwa ubunifu mkubwa kulinganisha na ambao nilishawaona katika media mbalimbali nilizowahi kuzitembelea.”
Aliwashauri Watanzania wanunue magazeti ya Global Publishers ambayo ni Amani, Risasi Mchanganyiko, Uwazi, Ijumaa Wikienda, Championi na Spoti Xtra ili kujionea uhondo uliomo.
(PICHA: SWEETBERT LUKONGE | GLOBAL PUBLISHERS)
Comments are closed.