Barcelona Yatwaa Super Cup, Hizi Hapa Rekodi Alizoweka Messi
KLABU ya Barcelona imefanikiwa kutwaa Kombe la Spanish Super Cup baada ya kuichapa Sevilla kwa bao 2 – 1 mchezo uliyopigwa Tangier nchini Morocco.
Katika mchezo huo, ikiwa ni game yake ya kwanza tangu akabidhiwe unahodha wa Barcelona kutoka kwa Andres Iniesta, Lionel Messi ameweka rekodi yake ya kutwaa mataji mengi zaidi ndani ya timu hiyo kuliko mchezaji yeyote mara baada ya kufikisha idadi ya makombe 33.
Sevilla ilitangulia kupata bao mapema kupitia kwa Pablo Sarabia kisha Barça kusawazisha kupitia kwa Gerard Pique kabla ya Ousmane Dembele kuipatia timu hiyo ushindi kwa goli lake la dakika za mwiaho.
Comments are closed.