The House of Favourite Newspapers

Beki wa Manchester City Ashtakiwa kwa Ubakaji

0

BEKI wa Manchester City na timu ya taifa ya Ufaransa , Benjamin Mendy (27) ameshtakiwa kwa makosa manne ya ubakaji na lingine la unyanyasaji wa kijinsia, Polisi wa Cheshire wamethibitisha.

 

Makosa hayo yanawahusu walalamikaji watatu walio na umri wa zaidi ya miaka 16 na yanaelezwa kufanyika kati ya Oktoba 2020 na Agosti mwaka huu.

 

Klabu ya Manchester City imesema mlinzi huyo, ameondolewa kwenye kikosi ili kupisha uchunguzi wa kesi yake hiyo.

 

“Suala hilo liko kwenye mchakato ya kisheria kwa hivyo klabu haitaweza kuzungumzia zaidi mpaka litakapokamilika,” Klabu hiyo iliongeza

Leave A Reply