The House of Favourite Newspapers

BELLE 9: NDOA HAIWEZI KUNIPOTEZA KIMUZIKI

MWANA-MUZIKI anayetamba na Ngoma ya Mfalme, Abednego Damian ‘Belle 9’ ambaye hivi karibuni aliingia kwenye ndoa ameibuka na kusema hawezi kupotea kimuziki kisa kuoa kama wasanii wengi wanavyokuwa.

 

Akizungumza na Showbiz-Xtra, Belle 9 alisema, yeye ni msanii anayejiamini kwenye kazi zake hivyo hawezi kutetereka sababu ya ndoa, akashuka kimuziki kama ilivyotokea kwa wasanii wengine.

 

“Suala la kushuka kimuziki kisa ndoa sikubaliani nalo hata kidogo, hao wanaoshuka wanashuka kwa sababu zao binafsi, sidhani kama sababu ni ndoa, kwanza huyu mwanamke ninaye siku nyingi vipi nifeli baada ya kumuoa,”alisema.

MAYASA MARIWATA

Comments are closed.