The House of Favourite Newspapers

Benki ya Biashara ya DCB yang’ara tuzo za NBAA

Mkurugebzi wa Fedha wa DCB, Zacharia Kapamba (katikati) akionyesha tuzo ambayo benki hiyo imeshinda, muda mfupi baada ya kukabidhiwa na naibu waziri wa fedha. Pamoja naye ni baadhi ya wafanyakazi wa benki hiyo.
Mkurugenzi wa Fedha wa Benki ya Biashara ya DCB, Zacharia Kapama (kulia) na Mkuu wa Kitengo cha Udhibiti Utendaji cha DCB, Siriaki Kiriki, wakionyesha tuzo ambayo benki hiyo imeshinda katika kitengo cha benki ndogo ngodo na za kati katika tuzo za  Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu (NBAA).
Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Dk. Ashatu Kijaji (wa tatu kushoto) akikabidhi tuzo ya ushindi wa pili katika kitengo cha benki ndogo na za kati katika tuzo za Mwasilishi Bora wa Hesabu za Bodi ya Wahasibu na Wakaguzi  wa Mahesabu (NBAA) kwa mwaka 2017 kwa Mkurugenzi wa Fedha wa Benki ya Biashara ya DCB, Zacharia Kapama, katika hafla iliyofanyika jijini Dar es Salaam juzi. Wa pili kushoto ni Mwenyekiti wa Bodi ya NBAA, Prof. Isaya Jairo.

 

 

Benki ya Biashara ya DCB imeahidi kuendelea kubuni na kuboresha huduma na bidhaa zake hususani huduma za kidigitaji ili iendelee kungara katika tuzo zijazo za Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Mahesabu  (NBAA).

 

Hayo yalisemwa na Mkurugenzi wa Biashara wa benki hiyo, James Ngaluko,  mara baada ya benki hiyo kukabidhiwa tuzo za NBAA katika kipengele cha mabenki madogo na  ya ukubwa wa kati, katika hafla iliyofanyika jijini Dar es Salaam juzi.

Naye akizugumza katika hafla ya kupokea tuzo hizo, Mkurugenzi wa Fedha wa benki hiyo, Zacharia Kapama alisema wamekuwa wakishinda tuzo hizo kwa miaka mitatu mfululizo na hiyo imetokana na kuzingatia viwango vya kitaifa na kimataifa katika utoaji wa taarifa za usimamizi wa fedha.

 

Comments are closed.