Benki ya Walimu Waungana na Maxmalipo Kutoa Huduma
MWALIMU Commercial Bank (MCB) imeongeza matawi ya utoaji wa huduma za kibenki kwa kuwatumia mawakala wa Maxmalipo.
Mfanyakazi wa Maxmalipo akionyesha jinsi kadi za Benki ya Walimu zitakavyokuwa zikitumika kwenye mashine za Maxmalipo.
Hilo limetokana na uzinduzi wa mpango wa benki hiyo wa kuwatumia zaidi ya mawakala 16,000 wa Maxmalipo kutoa huduma zake za kibenki nchini.
Uamuzi huo umefikiwa katika mkutano mkuu wa wanahisa wa benki hiyo unaofanyika jijini Tanga leo, Juni 21, 2018.
Comments are closed.