Ikiwa ni siku ya 15 tangu kuanza kwa shindano la CAMON KAMA ZOTE Kampuni ya simu ya TECNO ilimtaja Bi Trophonia kuwa mshindi wa pikipiki wa shindano hilo la CAMON KAMA ZOTE katika msimu huu wa kwanza kupitia Lucky draw iliyofanyika katika duka la simu la TECNO lililopo Mlimani City na kurushwa live kuitia kurasa yao ya @tecnomobiletanzania, ikiwa imejumuisha maduka yote yenye promotion jijini Dar es Salaam, Mwanza, Tabora, Arusha, Mbeya na Dodoma.
Mshereheshaji wa hafla hiyo ambaye ni Ofisa wa digital TECNO, Bi Salma Shafii, katika hafla hiyo alimkaribisha msanii maarufu wa comed Dully Vanny kuchezesha lucky draw.
Baada ya kumalizika kwa burudani kutoka kwa msanii huyo kampuni hiyo kuitia Afisa Masoko wa Kampuni ya simu ya TECNO Bwana Moses Mtweve, ilimtangaza Bi Trophonia kuwa mshindi na kuahidiwa kupelekewa pikipiki hiyo hadi anapoishi.
Lakini pia haikuishia hapo washindi wengine waliopatikana kupitia kipengele cha maswali na majibu ambao ni Agyprecious Emanuel, Kitongo Nuru, Cluzy Eyes na Ally Famadi ambao wote kwa pamoja walijishindia stand ya simu, mpira wa TECNO, T-shirt ya TECNO na chupa.
TECNO inaendelea kuwakumbusha wateja wake kufika kwenye madu yake na kununua simu za TECNO CAMON Series ili kuingia katika droo ya pili ya pikipiki na zawadi nyingine kemkem.
Kwa habari nyingi zaidi tembelea http://www.tecno-mobile.com/tz/index.php?id=740#/
Comments are closed.