BODI ya Filamu nchini imesema kauli iliyotolewa na Mbunge wa Geita Vijijini (CCM), Joseph Kasheku ‘Msukuma’, inaidhalilisha bodi hiyo na wasanii.
Jana Musukuma alisema bungeni: ‘Tasnia ya filamu nchini ipo hoi taabani. Wasanii wa Bongo Movie hawana kitu, wanategemea michango ya misiba, kufungua madanguro na kuwa makuwadi wa wanaume.”
Hata hivyo, jana wasanii wa filamu za Kibongo nchini walisema wanajipanga kwenda jijini Dodoma kwa lengo la kumpongeza Msukuma kutokana na kupigania haki za wasanii wa tasnia hiyo.
Comments are closed.