TRAVIS SCOTT KULIPA MAMILIONI KWA KUTOFANYA SHOO
MWANAMUZIKI wa Marekani, Travis Scott, ametakiwa na mahakama kulipa Dola 382,932,79 (Tsh. millioni 880.5) baada ya kutotokea kwenye tamasha la muziki mwaka 2018
Hata, hivyo, mwanasheria wake amesema malipo hayo hayaendani na maandalizi ya shoo iliyokuwa imeandaliwa na mapromota mwaka huo.
Mwanamuziki huyo alilipwa pesa ya utangulizi (advance) kiasi cha Tsh. milioni 345.8 na usafiri wa ndege binafsi lakini aliishia kutofika kwenye shoo hiyo.
Hata hivyo, alijitetea kuwa hakutokea kwa sababu ya hali ya hewa
Comments are closed.