The House of Favourite Newspapers

Breaking: Aliyetuhumiwa Kumteka Mo Dewji Aachiwa Huru

0

 

Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam imemfutia kesi na kumwachia huru dereva taksi Mousa Twaleb aliyekuwa akituhumiwa kuhusika na tukio la kutekwa kwa mfanyabiashara maarufu, Mohammed Dewji almaarufu ‘Mo Dewji’.

 

Twaleb alipandishwa kizimbani kwa mara ya kwanza Mei 28, 2019 akikabiliwa na mashtaka matatu likiwemo la kumteka Mo, tukio lililotokea alfajiri ya Oktoba 11, 2018 wakati mfanyabiashara huyo akielekea mazoezini katika Hoteli ya Colosseum iliyopo Oysterbay jijini Dar es Salaam.

 

Bilionea huyo aliachiliwa huru Oktoba 20, 2019 zikiwa ni siku tisa baada ya kutekwa baada ya watu waliomteka kudaiwa kumtelekeza kwenye viwanja vya Gymkhana.

@manyota_rich

Leave A Reply