SIMANZI na vilio vilitawala jana wakati wa mazishi ya Mkuu wa Shule ya Sekondari Migukulama iliyopo Kata ya Nyanzenda Halmashauri ya Buchosa wilayani Sengerema., Benedicto Lweikiza (45) aliyefariki kwa kujinyonga akiwa chumbani kwake na kuzikwa kijijini kwao Kasisa wilayani humo.
Katika msiba huo uliohudhuriwa na mamia ya wananchi, ndugu, marafiki , wanafunzi na walimu wenzake na marehemu uliibua hisia miongoni mwa waombolezaji huku wakieleza kusikitishwa kwao na uamuzi kwa mwalimu huyo kukatisha maisha yake ghafla.
Akizungumza na Global TV Online mara baada ya mazishi ya mwalimu huyo, Ofisa Elimu wa Sekondari Wilaya ya Sengerema, Benjamin Sperito alisema marehemu alikuwa mchapakazi na akijituma katika kutekeleza majukumu yake ya ualimu hivyo ameacha pengo kubwa katika tasnia hiyo kwani walimtegemea kwa mambo mengi.
Naye Mhandisi Benard Mtutuzi amabye ni mjomba wa marehemu alieleza namna walivyoshirikiana na Lweikiza katika mambo mbalimbali hasa ya ujenzi wa Taifa huku akieleza kuwa hatomsahahu mwalimu huyo kwa utendaji wake wa kazi mzuri uliotukuka.
Aidha Mtutuzi amewasihi wananchi wengine kutumia busara katika kufanya maamuzi ili yasije yakagharimu maisha yao na jamii inayowazunguka.
Aidha watoto wa Marehemu ambao ni Fredy Lweikiza na Frank Lweikiza (14) walieleza namna walivyopokea kwa masikitiko taarifa za kifo cha baba yao.
“Shangazi alikuwa anapika, alipoivisha akawa amekwenda kumuangalia baba, lakini akakuta ananing’inia dirishani ndipo akaja kuniita, baada ya kuchungulia dirishani nikamuona baba akiwa amekata roho tukamuita Fredy pamoja na majilani na walimu wengine wakawa wamefika”, alisema Frank.
Watoto hao walionekana kuwa wenye simanzi kubwa kwani mama yao nay7e alishafariki miaka mitano iliyopita.
Lweikizaalifariki kwa kujinyonga Septemba 9, saa tisa alasiri katika Mtaa wa Kilabela Kata ya Nyatukala wilayani Sengerema mkoani Mwanza.
nn
NA IDD MUMBA | GLOBAL TV, MWANZA.