Naibu Spika, Dkt. Tulia Ackson ameahirisha shughuli za Bunge leo Jumatatu mpaka kesho, saa 3 asubuhi kupisha maombolezo ya msiba wa Mbunge wa Jimbo la Buyungu (CHADEMA), Kasuku Bilago aliyefariki juzi Jumamosi Mei 26, katika Hospitali ya Taifa Muhimbili alipokuwa akitibiwa.
Mwili wamarehemu unatarajiwa kuagwa kesho Jijini Dodoma na wabunge wote kabla ya kusafirishwa kwenda kwao Kigoma kuzikwa..
Comments are closed.