Chadema Yashinda Umeya Ilala-Dar
Meya Mteule wa Ilala, Charles Kuyoka (Chadema) akiongea baada ya kushinda (aliyesimama wa pili kushoto).Mwenyekiti wa Chadema Taifa, Freeman Mbowe akizungumza na wanahabari.
Naibu Katibu Mkuu wa CUF, Magdalena Sakaya akizungumza na wanahabari.
Uchaguzi wa meya wa halmashauri wa Ilala jijini Dar es Salaam umefanyika leo ambapo Charles Kuyoka (Chadema) ameshinda umeya Ilala kwa kura 31 na Naibu Meya ni Omary Kumbilyamoto (CUF), aliyeshinda nafasi hiyo kwa kupata kura 31.
Madiwani wa Chama cha Mapinduzi (CCM) hawakupiga kura kutokana na madiwani kutoka Zanzibar kukataliwa kuingia ukumbini kupiga kura.
(PICHA: DEOGRATIUS MONGELA/GPL)