The House of Favourite Newspapers

CHADEMA YAONYA KUHUSU WALIOSHIKWA KWENYE MAANDAMANO

Kaimu Katibu Mkuu  wa Chama cha  Demokrasia na Maendeleo (Chadema), John Mnyika,  akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam.
Mkutano na waandishi wa habari ukiendelea.
Baadhi ya waandishi wa habari waliokuwa katika mkutano huo.

 

MBUNGE  wa Jimbo la Kibamba na Kaimu Katibu Mkuu  wa Chama cha  Demokrasia na Maendeleo (Chadema), John Mnyika,  amesema jeshi la polisi lisipowapatia dhamana leo wananchi 40 waliokamatwa katika maandamano ya  Februari 16 mwaka huu wakati wakielekea ofisini kwa Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi  Kinondoni kuanzia kesho, wataenda mahakamani kwa ajili ya kupatiwa sheria inayoruhusu jeshi la polisi kuwashikilia kwa muda wote huo.

 

Amesema kuwa kitendo cha jeshi la polisi kuwashikilia kwa muda wote huo  ni ukiukwaji wa sheria na haki za binadamu, hivyo chama chao kipo tayari kufungua kesi dhidi ya polisi.

 

Mnyika alifafanua kwamba wamefanya uchunguzi na wamebaini miongoni mwa wananchi hao waliokamtwa si wafuasi wa Chadema bali raia waliokuwa wakipita njiani na kukumbwa na balaa hilo ambapo wengine ni watoto wadogo walio chini ya umri wa miaka 18.

 

NA DENIS MTIMA/GPL

Comments are closed.