The House of Favourite Newspapers

Chama Cha Maofisa Uhusiano Chazinduliwa Dar

0
Rais wa Chama Cha PRST, Loth Makuza akizungumza jambo.
Meza kuu ilivyoonekana.
Msaidizi wa Mkurugenzi wa Idara ya Habari( MAELEZO), Jonas Kamaleki akipokea cheti cha Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu Benjamin Mkapa, kutokana na mchango wake wa kuagiza idara za serikali kuwa na msemaji.
Baadhi ya wageni waalikwa waliohudhuria hafla hiyo.
Mwakilishi wa Umoja wa Ulaya, Suzan Mbise  aliyekuwa mmoja wa wageni waalikwa akizungumza jambo.
Wakiwa katika picha ya pamoja.

CHAMA Cha Maofisa Uhusiano wa Umma (PRST) kimezinduliwa jijini Dar es Salaam, ambapo maudhui makubwa ya kuundwa kwa umoja huo ni kutambulika rasmi kama taasisi na kupanuana mawazo ya utumishi miongoni mwa wanachama, ikiwa ni pamaoja na kuendesha shughuli zao kwa utaratibu maalum.

Akihutubia katika uzinduzi huo, mgeni rasmi ambaye ni Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Ndege Makula aliwasisitizia wanachama juu ya kudumisha maadili ya umma katika utumishi wao huku akitilia mkazo suala la kujali misingi ya taaluma na matakwa ya sheria katika kulitumikia taifa.

“Nawaomba mtambue kuwa kupitia ummoja wenu huu ninyi mmebeba dhamana kubwa ya kuhakikisha mnatumika ipasavyo kwa wananchi, kwa hiyo cha muhimu ni kuzingatia maadili na misingi ya taaluma yenu ikiwa ni pamoja na kufuata sheria inataka nini, vinginevyo niwatakieni utumishi mwema katika nafasi hizi muhimu kwa jamii,” alisema Makula.

Leave A Reply