The House of Favourite Newspapers

Chongolo Afunguka “CCM Tunataka Katiba Iliyo Bora”

0
Katibu Mkuu  wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Taifa Mhe. Daniel Chongolo akisalimiana na baadhi ya viongozi wa kimila waliofika kumpokea Wilayni Mufindi
Wananchi wa Wilaya ya Mufindi wakiwa na bango lao la mapokezi ya Katibu Mkuu CCM, Daniel Chongola katika wilaya hiyo.
Katibu Mkuu wa CCM, Daniel Chongolo  akizungumza jambo na Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Mufindi ,Daud Yasin mara baada ya kuwasili kwenye ofisi za chama hicho Wilayani Mufindi
Katibu Mkuu wa CCM, Mhe. Daniel  Chongolo akisalimiana na Mbunge wa jimbo la Isimani Mhe,William Lukuvi pamoja na wageni wengine waliompokea
Katibu wa NEC Oganaizesheni Ndugu Issa Ussi Gavu akiwasalimia baadhi ya Wanachama wa CCM na Wananchi waliofika kuwapokea.
Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Ndugu Sophia Mjema akizungumza jambo. Kulia kwake ni Katibu wa NEC Oganaizesheni Ndugu Issa Haji Gavu.
Katibu mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Daniel Chongolo akizungumza mbele ya Wanachama,wafuasi wa chama hicho pamoja na Wananchi (hawapo pichani) alipowasili wilayani Mufindi mkoani Iringa kuanza ziara yake ya Siku 7 inayolenga kuimarisha uhai wa Chama kuanzia ngazi za Shina, kukagua utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2020-2025, pamoja na kusikiliza kero za wananchi

Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Daniel Chongolo amesema kwa sasa hakuna chama chochote cha Siasa au Mtu yeyote aliye na uhitaji mkubwa wa Katiba iliyo bora na yenye manufaa kwa Watanzania kuliko CCM.
Katibu Mkuu huyo  ametoa kauli hiyo leo Mei 26, 2023 wakati alipowasili wilayani Mufindi mkoani Iringa wakati akizungumza na Wanachama,wafuasi wa chama hicho pamoja na wananchi ikiwa ni siku ya kwanza ya ziara yake ya siku saba inayolenga kuimarisha uhai wa chama kuanzia ngazi za Shina, kukagua utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2020-2025, pamoja na kusikiliza kero za wananchi ili zipatiwe ufumbuzi.

“Nimesikia sikia huko watu wanasema sema kuhusu katiba mpya, labda niwaambie tu kwamba CCM tunahitaji katiba iliyobora kuliko mtu yoyote yule, ndio Maana Chama cha Mapinduzi kimempa ridhaa na dhamana Mwenyekiti wake Mhe. Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kuanzisha mchakato wa mapitio kuhusiana na suala la katiba mpya” amesema Chongolo.

Mhe. Chongolo amewasili Mafinga, wilaya ya Mufindi mkoani Iringa tayari kuanza ziara ya siku saba akiwa ameongozana na Wajumbe wawili wa Sekretarieti ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa, Katibu wa NEC Oganaizesheni Ndugu Issa Ussi Gavu na Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Ndugu Sophia Mjema.

Leave A Reply